SHIRIKA la Shina Inc la nchini Marekani na Tanzania,limetambulisha blanketi la kuulia wadudu wasumbufu na wale wanaosambaza maradhi kama mbu, chawa na kunguni.
alisema mablanketi hayo yamethibitishwa kwa majaribio mbalimbali kuwa ni salama kwa binadam, hivyo kwa hapa nchini wamekuja na blanketi 1100 kwa ajili ya kusambaza kwa ajili ya majaribio na kupata mrejesho.
Alisema hapa nchini wameanzia mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Mwanza, Kagera, Pemba na Unguja na baada ya hapo wataangalia mrejesho watakaoupata kabla ya kusambaza nchi nzima.
Aliongeza kuwa juu ya blanketi hilo mbu hawezi kuruka juu ya futi tano kwenye blanketi hilo. alisema matumizi yake ni kujifunikia wakati wa kulalia ama ukiwa unatembea.
Blanketi hilo lina teknolojia ya kisasa, utafiti wake umefanywa kwa miaka 25 kabla ya kuanza kutumika. zinatumika kwa nchi 40 duniani.
No comments:
Post a Comment